Hormonal imbalance ni hali ambapo kuna uzidifu au upungufu wa homoni moja au zaidi katika mwili, hali ambayo inaweza kusababisha matatizo mbalimbali ya kiafya. Ni neno pana ambalo linaweza kuelezea hali tofauti tofauti kuhusiana na homoni. Dalili za kawaida ni kama mabadiliko ya uzito, kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa, na chunusi na inategemea ni homoni ipi isiyo na uwiano.
Homoni ni kemikali zinazoratibu matendo mbalimbali ndani ya mwili kwa kusambaza ujumbe kupitia damu hadi kwenye viungo, ngozi, misuli na tishu nyingine. Ishara hizi huviambia viungo vya mwili nini cha kufanya na lini kifanyike. Homoni ni za muhimu kwa maisha na afya yako
Wanasayansi wamezitambua homoni zaidi ya 50 zilizomo ndani ya mwili hadi sasa.
Homoni na tishu nyingi (hasa viungo) vinavyozalisha na kuachia homoni vinaunda endocrine system.
Homoni hudhibiti shighuli nyingi katika mwili ikiwa ni pamoja na:
. Shughuli za ujenzi na uvunjaji wa seli za mwili (metabolism)
. Homeostasis (constant internal balance)
. Ukuaji
. Shughuli za mapenzi
. Uzazi
. Mzunguko wa kuamka na kulala (sleep-wake cycle)
. Hisia.
Hormonal Imbalance Ni Nini?
Hormonal imbalance ni hali inayotokea pale unapokua na homoni moja au zaidi nyingi zaidi au pungufu zaidi ya kiwango.
Homoni ni ishara zenye nguvu kubwa. Kwa homoni zilizo nyingi, kuzidi kidogo au kupungua kidogo tu kunaweza kuleta mabadiliko makubwa katika mwili wako na kupelekea hali fulani ambazo zitadai matibabu.
Hormonal imbalance nyingine ni za muda mfupi wakati nyingine zinaweza kuwa sugu (za muda mrefu). Isitoshe, hormonal imbalances nyingine zitahitaji tiba ili kurudia afya yako, wakati nyingine hazitaathiri afya yako bali tu kuzorotesha ubora wa maisha yako.
Hormonal Imbalance Inaweza Kusababisha Hali Zipi?
Hormonal imbalance inaweza kuleta mabadiliko ya kiafya ya aina nyingi sana katika mwili. Nyingi katika homoni, kuwa na uwingi wa kuzidi au kuwa na upungufu huleta dalili na matatizo ya kiafya. Wakati matatizo mengi yanayoletwa huhitaji tiba, mengine huweza kuondoka yenyewe.
Hali zinazoonekana mara nyingi na zinazosababishwa na hormonal imbalance ni:
. Hedhi zisizotabirika (irregula menstrual periods): Homoni kadhaa zinahusika katika mzunguko wa hedhi. Kwa sababu hiyo, kukosekana kwa uwiano katika moja au baadhi ya homoni kunaweza kusababisha hedhi zisizotabirika. Hali ambazo zinahusiana na homoni zinazosababisha hedhi zisizotabirika ni pamoja na polycystic ovary syndrome na amenorrhea.
. Kutopata mimba (infertility): Hormonal imbalance ni sababu inayoongoza ya ugumba kwa wanawake. Matatizo yanayohusiana na homoni kama ya PCOS na Kushindwa kupevusha yai (anovulation) huweza kusababisha ugumba. Wanaume nao pia huweza kupata tatizo la hormonal imbalance ambalo litasababisha ugumba, kama kuwa na kiwango cha chini cha testosterone (low testosterone levels – hypogonadism).
. Chunusi: Chunusi husababishwa kimsingi na vijitundu vilivyoziba. Pamoja na kuwa kuna vipengele vingi vinavyosababisha chunusi, mabadiliko ya homoni na hasa wakati wa kubalehe, yana mchango mkubwa. Tezi za mafuta, pamoja na zile za kwenye ngozi ya soni wako, husisimuliwa wakati homoni zikianza kufanya kazi ukiwa kwenye balehe.
. Hormonal acne (adult acne: Hormonal acne (adult acne) ni aina aya chunusi zinazotokea wakati mabadiliko ya homoni yanaongeza kiwango cha mafuta yanayotengenezwa na ngozi. Hii hutokea hasa wakati wa ujauzito, kukoma hedhi na watu walio kwneye tiba ya homoni (testosterone therapy).
Kisukari: Hali ianayaooneka mara nyigni ziadi inayotokana na homoni ni kisukari. Kisukari maana yake kongosho halitengenezi au linatengeneza homoni ya insulin kwa kiwango kidogo au mwili wako hauitumii insulin ipasavyo. Kuna aina kadhaa za kisukari. Aina zilizozoeleka zaidi ni Type 2 diabetes, Type 1 diabetes na gestational diabetes. Kisukari huhitaji tiba.
Thyroid disease: Kuna aina mbili za maagonjwa ya tezi dundumio nayo ni hypothyroidism (viwango vya chini vya homoni ya thyroid) na hyperthyroidism (viwango vya juu vya homoni ya thyroid). Kila moja ina sababu kadhaa. Magonjwa ya thyroid yanahitaji tiba.
Unene: Kuna homoni nyingi zinazohusika katika kuuambia mwili wako kuwa unahitaji chakula na namna mwili wako unavyotumia nishati , hivi kwamba kukosekana kwa uwiano wa baadhi ya homoni kunaweza kusababisha kuongezeka kwa uzito wa mwili (unene) kama naman ya hifadhi ya mafuta. Kwa mfano, kuwa na ziada ya homoni ya cortisol na kiwango cha chini cha homoni ya thyroid kunaweza kuchangia unene wa mwili.
Dalili Na Chanzo Cha Hormonal Imbalance
Ni Dalili Zipi Za Hormonal Imbalance
Kwa sababu mwili wako hutengeneza homoni tofauti yapata 50 – zote zikiwa na mchango mkubwa katika utendaji kazi wa mwili wako – unaweza kuona dalili tofauti kutegemeana na ukosefu wa uwiano wa homoni husika.
Yafaa kujua kuwa nyingi ya dalili hizi zinaweza kiusababishwa na vitu vingine, na si lazima kuwa ni tatizo la hormonal imbalance.
Hormonal Imbalance Inayoathiri Shughuli Za Kimetaboliki
Hormonal imbalance zinazoonekana kwa wingi ni pamoja na zile zinazoathiri shughuli za kimetaboliki ndani ya mwili wako. Shughuli za kimetaboliki ni mabadiliko ya kikemikali yanayotokea katika seli za mwili wako na kukibadilisha chakula kuwa nishati. Kuna homoni nyingi zinazohusika katika shughuli hizi.
Dalili za Hormonal Imbalances Zinazoathiri Shughuli Za Kimetaboliki
. Mapigo ya moyo kuwa chini au juu (tachycardia)
. Kupungua au Kuongezeka unene bila maelezo
. Uchovu
. Kufunga choo
. Kuharisha au kwenda haja kubwa mara kwa mara
. Ganzi au vitu kucheza kwenye mikono
. Viwango vikubwa mno vya cholesterol
. Mfadhaiko au wasiwasi
. Kushindwa kuhimili joto la juu au la chini
. Ngozi au nywele kavu vinavyokwaruza
. Ngozi nyembamba, ya joto na yenye unyevu
. Mafuta ya mwili kujipanga bila mpangilio
. Weusi wa ngozi kwenye makwapa au nyuma na upande wa kulia na wa kushoto wa shingo (acanthosis nigricans)
. Vitu vidogo kuota juu ya ngozi (skin tags)
. Kiu kali na kukojoa mara kwa mara.
Hormonal Imbalance Za Mapenzi Kwa Wanawake